Waambie, ewe Mtume, Qurani haikuzuliwa na mimi, bali aliyeiteremsha ni Jibrili kutoka kwa Mola wako kwa ukweli na uadilifu ili kuwafanya Waumini wawe imara, kuwaongoza wao kutoka kwenye upotevu , na kuwapa bishara njema wale waliojisalimisha na kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu, Bwana wa viumbe wote.