Tell the disbelievers that if they desist, their past will be forgiven. But if they persist, then they have an example in those destroyed before them.
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qiraat
Hadith
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wale waliokanusha upweke wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Washirikina wa watu wako kwamba watakomeka na ukafiri na kumfanyia uadui Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, na wakarudi kumuamini Mwenyezi Mungu Peke Yake na kutompiga vita Mtume na Waumini, Mwenyezi Mungu Atawasamehe madhambi yaliyopita, kwani Uislamu unafuta yaliyopita. Na watakaporudia washirikina hawa kukupiga vita baada ya tukio ambalo ulipata ushindi juu yao siku ya Badr, basi mwendo wa watu wa mwanzo umetangulia, nao ni kwamba wao wakikanusha na wakaendelea kwenye ukaidi wao, tutawaletea adhabu na mateso kwa haraka.
He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel